Nje ya Lango
by Florence Mureithi
Nitamfuata nje ya lango,
Nikifurahia aibu ya msalaba.
Aliyoibeba Mwanakondoo,
Nitamfuata nje ya lango la mji
Nitamfuata nje ya lango,
Aliyefanyika dhabihu kwa msalaba.
Alipoangikwa Mwanakondoo,
Nitamfuata nje lango la mji
Ameingia, mahali patakatifu,
Kwa Damu Yake, tuna ukamilifu.
Ameingia, mahali patakatifu,
Kwa Damu Yake, tuna ukamilifu
Ameyachukua,
Masikitiko yetu.
Amejitwika,
Huzuni zetu.
Kajeruhiwa,
Kwa makosa yetu.
Alichupuliwa,
Kwa maovu yetu